Saturday 20 July 2013

WASWAHILI NA KISWAHILI

Kabila lolote ulimwenguni, hutokana na mambo mane (manne) yakiwemo jadi, Kazi, mji na sifa za watu. Na upande mwengine nayo lugha hutokamana na mazingira maalum ya watu na utamaduni wao.  Ikiwa kabila ni desturi na mila za watu, au ni watu walofungamana na kuwa na tabia na nyendo ambazo zitawatofautisha wao na watu wengine, basi waswahili wana mila zao na desturi zao kama makabila mangine(mengine) ulimwenguni. Kama kwenye maingiliano ya kibinadamu k.m ndoa, majina, itikadi za pepo na kadhalika, basi liko kabila la waswahili lenye mambo kama hayo.

Kabila la waswahili, utamaduni wao, na lugha yao hupatikana ile sehemu y anti (nchi) iliyopatikana na maji ya pwani na mwambao wa Afrika mashariki. Wenye urefu wa kilomita 1500 pamoja na visiwa vilivyopakana na mwambao wenyewe.  Kiswahili ni lugha iliyotapakaa na kujulikana kote ulimwenguni na hata kuliko lugha nyengine yoyote ya Afrika.

Kuna rai kuwa neon “waswahili” lilitokea pale Muhammad Bin Abdallah Ibn Batuta na wasafiri wenzake walofika miji ya mwambao mwaka 1331 B.K. na kummuliza kijana wa kingozi, “Man ha ulaii”? kuwa wao kina nani? Akawajibu sisi ni As- Sawahili yaani wenyeji wa pwaa hizi.  Sahil ni neon la asili ya kiarabu na wingi wake sawahil yaani pwani (upwa) na watu wa bara arabu wakakwita huku Al-Sahili au as-sawahiliyy na wengine hudai neon “waswahili” latokana “wa-ziwa-hili”
Lakini kabla ya ya kuja ibn Batuta watu hao walikuwa wakiitwa wangozi, kutokana na mapokezi ya wazee wa kale wa Mombasa (Mfunzi) ni kua watu hawa walikuwa wakipima mashamba kwa vipande vya ngozi.  Kasha jina hilo likabadilika na kuitwa wavisai ama wakisai kwa kuwa walikuwa ni watu wakutoa visa na mwisho ndiyo kuitwa Waswahili.  
Lifwatalo ni shairi la kingozi limetungwa na Ustadh Ahmad Juma Bhalo (Ustadh Bhalo)

Mwanzimle mlekele, ni mwina wa bangu moyo
Moyo mtipi wa male, yasofupika maziyo
Maziyo maku si mbale, maningayo sifumbile
Siyo ndmi si nga soyo, maningayo simbile
(Taa ya Umalenga u.k 22)

Licha ya Waswahili kuwa wenyeji wa kitambo kuliko makabila mengine kwa mwenye kuelewa tarekhe (histria) vizuri.  Kinachosikitisha na kushangaza ni kwamba kuwa lugha hii tukufu nay a kale ni ya kigeni,  yaani asili yake si Afrika.  Wanao shika kani (kulitiliya nguvu jambo) na kulipigiya upatu suala hilo si rahisi kutamka fikra zao, kwa kucheleya kuthibitisha kuwa ni wajinga wa histria ingawa Kiswahili kimethibitishwa kuwa ni lugha asili ya kiafrika bila kusaza shaka yoyote.

Kuna na wenye fikra ya kuwa utamaduni wa Kiswahili ni wa kigeni, na kupinga kuwepo kwa watu waitwao waswahili kwa kusingizia kuwa maneno ya Kiswahili mangi (mengi) yamefanana na kiarabu.  Dai hilo tukilipima vizuri tutaona halina mashiko maana takriban lugha zote ulimwenguni zimeazimana maneno. Kwa mfano hebu tutizame kiingereza kilivyoazima maneno kutoka lugha ya Kiarabu.

Na maneno yenyewe ni kama yafwatayo;

      1.       Amber                                                  (anbar)
         2.       Crimson                                               (Karmazi)
        3.       Elixir                                                       (ikseer)
      4.       Carat                                                     (Kirat)
        5.       Cotton                                                  (al-Kutn)
        6.       Sherbet                                               (Sharabat)
      7.       Tahini                                                     (tahina)
8.       Clipher  /zero                                       (sifr)
      9.       Mask/mascra                                     (mascara)
        10.   Alcohol                                                 (al-kohool)
11.   Hazard                                                  (zahr)
 12.   Caliber                                                  (kaleb)
    13.   Jar                                                          (Ka’leb)
14.   Jar                                                          (jarra)

BASI KWANINI KIZUNGU KISIAMBIWE NI KIARABU LAKINI KISWAHILI KUWA NI KIARABU??

Na ale wanaokubali kuwepo kwa waswahili hutiya ila na kusema ati si kabila safi, na imetanganya (imechanganya) yaani kuambiwa Kiswahili ni lugha ya kigeni hapa Afrika mashariki. Madai haya yalizuka tu baada ya Africa kutawaliwa na waingereza, maana kabla ya ukoloni hapakuwako na shaka yoyote juu ya kuwepo kwa waswahili, wala lugha yao wala utamaduni wao. 

 Tete hizi za tuhuma za waswahili zilianza kuwashwa wakati wa ukoloni wa kiingereza, na zikabiririka zaidi pale nchi za Afrika mashariki zilipokaribia kuwa huru.  Kwa mfano wazungu walikuwa hawakubali kuwa mwafrika ana ustaarabu au jambo lolote la kuweza kuonyesha ulimwengu umiliki wa jambo Fulani. Ndipo leo tukaambiwa kuwa miji ya Kiswahili ni ya kiarabu kwa ajili ya milango yaliotongwa (chongwa) kwa nakshi za kupendeza, mavazi, majumba na kadhalika lakini ukiwauliza mambo haya yanatoka wapi sehemu za Arabuni hakuna awezaye kukujibu.

Marejeo:

Shihabudin Chiragdin na Mathias Mnyapala;  Historia ya Kiswahili.
Ahmad Nassir Juma Bhalo;                           Taa ya Umalenga
Shihabudin Chiragdin;                                   Kiswahili tokea ubantu hadi ki – standard Swahili
John Ayto;                                                    Dictionary of foreign words in English
Shihabudin Chiragdin;                                    Kiswahili na wenyewe



BY NAJEEB AHMAD NASSIR JUMA BHALO

Cell No.                0729-906-761
E-mail                   nagibbhalo@yahoo.com

No comments:

Post a Comment